logo

TAMISEMI

Students

FR
Fred Kibanofred.kibano@tamisemi.go.tz

WARATIBU WA HUDUMA ZA MACHO WAASWA KUJUMUISHA HUDUMA ZA MACHO KWENYE BAJETI ZA HALMASHAURI

Waratibu wa huduma za macho kutoka Mamlaka za Serikali za Mitaa wameaswa kuendelea kujumuisha huduma za macho katika Mipango na Bajeti za Halmashauri ili kuhakikisha urahisi wa upatikanaji wa huduma bora za afya ya macho kwa wananchi.

Hayo yamesemwa na Dkt. Ernest Kisandu, ambaye alizungumza kwa niaba ya mratibu wa macho kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, katika kambi ya matibabu ya mtoto wa jicho inayoendelea katika Hospitali ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe.

Dkt. Kisandu alisisitiza kwamba kuendelea kwa mipango ya huduma za macho kwenye bajeti za Halmashauri kutasaidia kupunguza changamoto zinazohusiana na matatizo ya macho, hasa kwa watoto kwani itahakikisha huduma hizi kupatikana kwa watu wengi na kuifanya afya ya macho kuwa sehemu ya huduma muhimu za afya za jamii.

Naye Afisa wa Programu kutoka Hellen Keller International, Bw. Allen Lemilia, amesema kambi hiyo ya siku sita, imekuwa na mwitikio mkubwa kutoka kwa wananchi wa Halmashauri ya Mbozi na maeneo jirani na imepata ushiriki mkubwa kutoka kwa jamii na inatarajiwa kutoa huduma kwa watu wengi zaidi.

Kambi hiyo ya matibabu inaendeshwa kwa ushirikiano kati ya Ofisi ya Rais TAMISEMI, Wizara ya Afya, na wadau wa Helen Keller International, ina lengo la kufikia watu 720 wenye matatizo ya mtoto wa jicho, ambapo hadi sasa jumla ya watu 412 wamepatiwa huduma.

Comments

Please sign in to leave a comment.

Matangazo Muhimu

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Habari na Matukio

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Cookie

We use cookies to enhance your browsing experience, provide personalized content, and analyze our traffic. By clicking "Accept All Cookies", you agree to the storing of cookies on your device to improve site navigation, analyze site usage, and assist in our marketing efforts. To learn more about how we use cookies and to manage your preferences, please visit our Cookie Policy.
National Election Commission Logo

Uchaguzi 2025

Kura yako haki yako jitokeze kupiga kura