
Wakurugenzi wa halmashauri waelekezwa kuwasilisha majina ya watumishi wanaodai malimbikizo
OR-TAMISEMI
Naibu Waziri Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mhe. Zainab Katimba amewaelekeza wakurugenzi wa Mamlaka za serikali za mitaa kutengeneza mchanganuo na kubaini watumishi wangapi wanadai malimbikizo ya mishahara na yasiyo yamishahara na kuyawasilisha Utumishi kuhakikiwa na kupekwa hazina kwaajili ya malipo.
Ameyatoa maelekezo hayo bungeni Dodoma wakati akijibu swali la Mhe. Bonnah Kamoli mbunge wa Segerea kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa, aliyetaka kujua serikali inampango gani wa kulipa malimbikizo ya mishahara na marupurupu ya walimu.
Akijibu hilo Mhe. Katimba amesema “Naomba nitoe msisitizo huo na jana kwenye bajeti ya wizara ya utumishi maelekezo hayo yalitolewa na wizara hiyo na mpaka itakapo fika tarehe 31 Mei wakurugenzi wote wawe wamewasilisha majina hayo ya watumishi hao ambao wanadai malipo yao” Amesema
Aidha, akijibu kuhusu mazingira bora ya walimu Mhe. Katimba amesema serikali inaendelea kujenga nyumba za walimu ili walimu wapate mazingira mazuri ya kuishi na kufanyakazi kwa ufanisi.
Comments
Please sign in to leave a comment.
Matangazo Muhimu
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.
TANGAZO LA KUITWA KAZINI KWA WALIMU WA KUJITOLEA 128 SHULE ZA MSINGI 128 KWA AWAMU YA PILI GPE TSP
ORODHA YA WALIMU WA KUJITOLEA 128 GPE TSP AWAMU YA PILI
ADDITIONAL BEST INDICATORS 2025
BASIC EDUCATION STATISTICS 2025
Generic ESMP for CERC Interventions under DMDP2
Habari na Matukio
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.




