
WAGANGA WAKUU WA MIKOA HAKIKISHENI HOSPITALI ZA WILAYA ZINALEA VITUO VYA AFYA – Prof. NAGU
OR-TAMISEMI
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia afya Prof. Tumaini Nagu amewaelekeza Waganga Wakuu wa Mikoa (RMO`S) Kuhakikisha hospitali zote za Wilaya nchini zinalea vituo vilivyopo chini yao ili kufanikisha upatikani wa huduma bora za afya kwenye vituo vyote vya ngazi ya afya Msingi.
Prof. Nagu ametoa maelekezo hayo wakati wa ziara ya usimamizi shirikishi katika Hospitali ya Wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani yenye lengo la kuangalia upatikanaji wa huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa jamii katika Mkoa huo.
“Waganga Wakuu wa Mikoa wote hakikisheni huduma bora zinazotolewa katika hospitali za Wilaya, vivyo hivyo hospitali hizo zilee vituo vya afya vilivyopo chini yake navyo viweze kutoa huduma bora na vituo vya afya vitalea zahanati za maeneo husika” amesisitiza Prof. Nagu.
Aidha, Prof. Nagu amewapongeza watumishi wa hospitali ya Wilaya ya Mkuranga kwa uhamasishaji mkubwa kwa wananchi kushiriki katika uchangia mkubwa wa damu na kufanya kuwe na hazina ya kutosha ya damu.
“Tumeona kuna damu nyingi kwenye majokofu yenu ya kuhifadhia damu na kuna utunzaji mzuri, pia katika maabara yenu kumekuwa na mwitikio mkubwa wa wananchi kuchangia damu, hii imetokana na elimu ambayo mmekuwa mkiitoa kwa wananchi” alisema Prof. Nagu.
Pia, ameipongeza Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga kwa kuwa na maabara bora yenye ithibati ambayo inahakikishia ubora wa majibu ya vipimo hivyo kuwezesha matibabu sahihi.
Comments
Please sign in to leave a comment.
TANGAZO LA KUITWA KAZINI WAOMBAJI WA NAFASI YA AJIRA YA MKATABA WA MAAFISA LISHE
CHAGUO LA PILI KIDATO CHA TANO
ORODHA YA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO WALIOPANGWA AWAMU YA PILI MWAKA, 2025
TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI. (ORAL INTERVIEW)
Tangazo la kuitwa kazini ajira za TMCHIP 2025