
TARURA WABADILISHANA UZOEFU NA WAHANDISI SEKTA YA USAFIRISHAJI
Arusha
Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) inaendelea kishiriki katika mafunzo yenye lengo la kuimarisha usimamizi wa mikataba ya miradi ili kupunguza gharama na ucheleweshaji wa miradi.
Mafunzo hayo ya siku tano ambayo yamewaleta pamoja wadau muhimu katika Sekta ya Ujenzi wa Miundombinu ya barabara na usafirishaji pamoja na mambo mengine yanalenga kubadilishana uzoefu katika sekta hiyo muhimu kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini.
Mkurugenzi wa Barabara kutoka TARURA, Mhandisi Venant Komba amewasilisha mada ya namna TARURA inavyo tekeleza majukumu yake, mikakati inayotumika katika usimamizi wa miradi, teknolojia zinazotumika katika ujenzi wa Barabara na changamoto zilizopo katika utekelezaji wa miradi hasa kipengele cha mikataba ikiwa ni sehemu ya kutoa uzoefu wa Wakala huo katika eneo hilo muhimu.
Akizungumza wakati wa uwasilishaji Mhandisi Komba amesema moja kati ya vipaumbele walivyonavyo kama taasisi ni kujengea wataalamu wao uwezo (capacity building) hasa katika maswala ya usimamizi wa mikataba ili kuepusha changamoto wakati wa utekelezaji wa miradi.
“Tunatumia nafasi kama hizi kama fursa ya kuendelea kujifunza kutoka kwa wenzetu' amesema.
Mafunzo hayo yameandaliwa na Chama cha Barabara Tanzania (TARA) kwa kushirikiana Wahandisi washauri kutoka ndani na nje ya nchi.
Comments
Please sign in to leave a comment.
Matangazo Muhimu
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.
TANGAZO LA KUITWA KAZINI KWA WALIMU WA KUJITOLEA 128 SHULE ZA MSINGI 128 KWA AWAMU YA PILI GPE TSP
ORODHA YA WALIMU WA KUJITOLEA 128 GPE TSP AWAMU YA PILI
ADDITIONAL BEST INDICATORS 2025
BASIC EDUCATION STATISTICS 2025
Generic ESMP for CERC Interventions under DMDP2