logo

TAMISEMI

Students

FR
Fred Kibanofred.kibano@tamisemi.go.tz

TAMISEMI, BIG WIN PHILANTHROPY WAANDAA MPANGO JUMUISHI KUKABILIANA NA UDUMAVU NA KUBORESHA LISHE

Ofisi ya Rais TAMISEMI, kwa kushirikiana na Shirika la Big Win Philanthropy, wamefanya kikao kazi cha kuandaa Mpango Jumuishi wa utekelezaji wa Afua za Lishe kwa Mikoa ya Iringa, Tabora na Geita. Mikoa hiyo imechaguliwa kwa kuwa na idadi kubwa ya watoto walio na udumavu na waliochini ya umri wa miaka mitano huku lengo likiwa ni kuboresha hali yao ya lishe.

Kikao hicho kimeongozwa na  Bw. Mwita Waibe, ambaye ni Mratibu wa Mradi huo kutoka OR - TAMISEMI, Huku kikihudhuliwa na  Dkt. Taye Balcha, Mkurugenzi Mkuu wa Programu kutoka Shirika la Big Win Philanthropy,  Bw. Vikram Mand Meneja uendeshaji kutoka Big Win philanthropy, pamoja na Maafisa na washauri wa lishe kutoka Mikoa husika, wakiwa na lengo la kuweka misingi thabiti ya mpango huo muhimu.

Kwa pamoja, washiriki walijadili mikakati ya kuhakikisha kuwa programu inafikiwa kikamilifu na kuwafikia watu wanaolengwa. Hii inaendezeleza jitihada za Serikali za  kukabiliana na changamoto za lishe na udumavu kwa kutumia mbinu za ushirikiano imara.

Comments

Please sign in to leave a comment.

Matangazo Muhimu

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Habari na Matukio

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Cookie

We use cookies to enhance your browsing experience, provide personalized content, and analyze our traffic. By clicking "Accept All Cookies", you agree to the storing of cookies on your device to improve site navigation, analyze site usage, and assist in our marketing efforts. To learn more about how we use cookies and to manage your preferences, please visit our Cookie Policy.
National Election Commission Logo

Uchaguzi 2025

Kura yako haki yako jitokeze kupiga kura