
SALUM SIMBA BINGWA MCHEZO WA DRAFTI MICHEZO MEI MOSI 2025.
OR- TAMISEMI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan amemkabidhi kombe la ushindi wa mchezo wa drafti mtumishi wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Bw. Salum Simba baada ya kuibuka kinara wa mchezo huo kitaifa kwa upande wa wanaume.
Ushindi huo ameupata katika Mashindano ya Michezo ya Mei Mosi 2025 baada ya kushinda mchezo wa fainali hiyo na kupeperusha vema bendera Ofisi ya Rais-TAMISEMI katika mashindano hayo.
Rais Dkt. Samia alitoa zawadi kwa mshindi huyo leo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi iliyofanyika kitaifa katika uwanja wa Bombadia mkoani Singida.
Ushindi wa Simba katika mchezo hiyo unaonesha vipaji vya mchezo walivyonavyo watumishi wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI.
Comments
Please sign in to leave a comment.
TANGAZO LA KUITWA KAZINI KWA WALIMU WA KUJITOLEA 128 SHULE ZA MSINGI 128 KWA AWAMU YA PILI GPE TSP
ORODHA YA WALIMU WA KUJITOLEA 128 GPE TSP AWAMU YA PILI
ADDITIONAL BEST INDICATORS 2025
BASIC EDUCATION STATISTICS 2025
Generic ESMP for CERC Interventions under DMDP2