
Prof.Mkenda asisitiza umuhimu wa Elimu ya Amali kukuza ujuzi
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Prof. Adolf Mkenda, amesisitiza umuhimu wa elimu ya amali kama njia ya kukuza ujuzi wa kiutendaji katika sekta mbalimbali kama vile ufundi, kilimo, uvuvi, muziki na michezo.
Aidha, ametoa wito kwa wazazi na wawekezaji kuunga mkono elimu hiyo kwa kuwa ni suluhisho muhimu kwa changamoto ya ukosefu wa ajira na inahitajika kwa ufanisi wa sekta ya uwekezaji.
Prof. Mkenda ameyasema hayo , katika Mkutano wa Umoja wa Maafisa Elimu wa Mikoa na Halmashauri uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Ameeleza kuwa shule za amali zitakazokuwa na rasilimali na vitendea kazi vya kutosha zitapata kibali cha kufundisha na kutoa mafunzo ya vitendo.
Pia, amesisitiza kuwa elimu ya amali inapaswa kuimarishwa ili kukabiliana na upungufu wa wafanyakazi wenye ujuzi katika sekta mbalimbali za uchumi.
"Wazazi kumsihofie kupeleka watoto wenu katika shule za amali, elimu hii ni fursa muhimu ya kuwajengea watoto maisha bora na mustakabali mzuri wa ajira,"amesema.
Comments
Please sign in to leave a comment.
Matangazo Muhimu
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.
TANGAZO LA KUITWA KAZINI WAOMBAJI WA NAFASI YA AJIRA YA MKATABA WA MAAFISA LISHE
CHAGUO LA PILI KIDATO CHA TANO
ORODHA YA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO WALIOPANGWA AWAMU YA PILI MWAKA, 2025
TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI. (ORAL INTERVIEW)
Tangazo la kuitwa kazini ajira za TMCHIP 2025