
PROF. NAGU AHAMASISHA WANANCHI KUJIUNGA NA BIMA YA AFYA KOROGWE
Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI anayeshughulikia Afya, Profesa Tumaini Nagu, ameendelea kuwahamasisha wananchi kujiunga na Bima ya Afya ili kuondoa usumbufu wa gharama za matibabu.
Profesa Nagu amesema hayo wilayani Korogwe mkoa wa Tanga wakati akihitimisha ziara ya usimamizi shirikishi ya kutembelea vituo vya kutolea huduma za Afya na kuzungumza na watumishi katika maeneo ya kutolea huduma za Afya.
"Katika kuhakikisha huduma hizi za Afya zinaendelea ni muhimu wananchi waweze kugharamia na njia bora ya kugharamia huduma za afya ni kwa kuwa na bima tunatoa rai kwa wananchi wote kila mmoja na kila familia kujiunga na bima ya Afya ili wakati wa kupata changamoto fedha zisije kuwa kikwazo." amesema
Amewaomba watumishi kuwa mabalozi wa kuwahamasisha wananchi wanajiunga na Bima ya Afya kuanzia nyumbani hadi kwenye maeneo wanayotolea huduma.
Kwa upande wake, mkurugenzi wa Halmashauri ya Korogwe Mji, Bi. Mwashabani Mrope, amepokea maelekezo hayo na kusema Halmashauri hiyo itaendelea kutekeleza maagizo ya serikali kwa kuboresha huduma za Afya.
Naye Juma Mhina, mwenyekiti wa Kijiji cha Kwamsisi, ameishukuru serikali kwa ujenzi wa kituo cha Afya, kwani kinawasaidia kupata huduma kwa urahisi na haraka tofauti na mwanzo walipokuwa na jengo moja lililokuwa na ufanisi mdogo wa kutolea huduma.
Profesa Nagu yupo mkoani Tanga kwaajili ya ziara ya usimamizi shirikishi akiwa ambatana na wataalamu wa Afya kutoka Ofisi ya Rais – TAMISEMI lengo likiwa ni kuendelea kuhamasisha ubora wa huduma za Afya kwa wananchi.
Comments
Please sign in to leave a comment.
Matangazo Muhimu
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.
TANGAZO LA KUITWA KAZINI KWA WALIMU WA KUJITOLEA 128 SHULE ZA MSINGI 128 KWA AWAMU YA PILI GPE TSP
ORODHA YA WALIMU WA KUJITOLEA 128 GPE TSP AWAMU YA PILI
ADDITIONAL BEST INDICATORS 2025
BASIC EDUCATION STATISTICS 2025
Generic ESMP for CERC Interventions under DMDP2