logo

TAMISEMI

Students

FR
Fred Kibanofred.kibano@tamisemi.go.tz

MTWALE AHIMIZA LUGHA ZA STAHA KWA WATUMISHI WA SERIKALI ZA MITAA.

Na OR- TAMISEMI, Pwani

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – TAMISEMI anayeshughulikia Serikali za Mitaa, Sospeter Mtwale amewahimiza Wakuu wa Idara na Vitengo wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kutotumia lugha zisizo na staha kwa wananchi na watumishi wanaowasimamia.

Mtwale amesema hayo wakati wa kufungua mafunzo ya Uongozi kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa yalioratibiwa na Ofisi ya Rais – TAMISEMI kwa kushirikiana na UONGOZI INSTITUTE, ambayo yameanza leo tarehe 29 Agosti, 2025 katika Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Julius Nyerere kilichopo  ya Kibaha mkoani Pwani ambapo amehimiza kupunguza malalamiko yanayotolewa na watumishi wa ngazi za chini na wananchi.

“Tumezoea kupata mafunzo mara nyingi yanayohusu kada zetu tunazozisimamia katika kila idara, lakini mafunzo haya yamebuniwa kuwawezesha  Wakuu wa Idara na Vitengo kuwa na uwezo wa kiuongozi ili kutekeleza majukumu yenu kwa ufanisi na uadilifu,” amefafanua Mtwale.

Katika kusisitiza umuhimu wa uadilifu katika uongozi, Mtwale amesema mafunzo yanayotolewa yanalenga kuongeza uhodari na ujuzi katika utendaji wa kazi katika kutatua changamoto zilizobainika katika utekelezaji wa majukumu.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa mkoa wa Pwani, Pili Mnyema amesema mafunzo haya yatasaidia kubadilika kifikra na utendaji wa watumishi na amewasihi viongozi wanaopata mafunzo hayo kuwa kielelezo cha uongozi kwa wengine

Comments

Please sign in to leave a comment.

Matangazo Muhimu

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Habari na Matukio

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Cookie

We use cookies to enhance your browsing experience, provide personalized content, and analyze our traffic. By clicking "Accept All Cookies", you agree to the storing of cookies on your device to improve site navigation, analyze site usage, and assist in our marketing efforts. To learn more about how we use cookies and to manage your preferences, please visit our Cookie Policy.
National Election Commission Logo

Uchaguzi 2025

Kura yako haki yako jitokeze kupiga kura