
Msovela: Fanyeni Kazi Kama Timu Kuleta Maendeleo
Na Angela Msimbira, Pwani
Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, Albert Msovela, amewataka Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa ushirikiano na mshikamano ili kufanikisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika mikoa yao.
Akizungumza leo Mei 20, 2025, katika mafunzo ya uongozi kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa yanayofanyika katika Chuo cha Uongozi mkoani Pwani, Msovela amesema kuwa ushirikiano ni nguzo muhimu katika kufanikisha malengo ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuwaletea wananchi maendeleo ya haraka na yenye tija.
“Ni muhimu tufanye kazi kama timu moja. Miradi ya maendeleo haiwezi kutekelezwa kwa ufanisi ikiwa kila mmoja atafanya kazi kivyake. Ushirikiano, mawasiliano na uwajibikaji ni mambo ya msingi,” amesisitiza Msovela.
Aidha, ameongeza kuwa Makatibu Tawala Wasaidizi wanapaswa kuratibu kwa ufanisi shughuli zote za maendeleo, kufuatilia utekelezaji wake kwa karibu, na kutoa taarifa sahihi kwa wakati ili kusaidia serikali kufanya maamuzi yenye tija.
Msovela amesema viongozi hao ni kiungo muhimu kati ya wananchi na Serikali, hivyo ni lazima wawe karibu na wananchi, kusikiliza changamoto zao na kushirikiana nao katika kuzitafutia suluhisho la kudumu.
Comments
Please sign in to leave a comment.
TANGAZO LA KUITWA KAZINI WAOMBAJI WA NAFASI YA AJIRA YA MKATABA WA MAAFISA LISHE
CHAGUO LA PILI KIDATO CHA TANO
ORODHA YA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO WALIOPANGWA AWAMU YA PILI MWAKA, 2025
TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI. (ORAL INTERVIEW)
Tangazo la kuitwa kazini ajira za TMCHIP 2025