
Msovela: Fanyeni Kazi Kama Timu Kuleta Maendeleo
Na Angela Msimbira, Pwani
Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, Albert Msovela, amewataka Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa ushirikiano na mshikamano ili kufanikisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika mikoa yao.
Akizungumza leo Mei 20, 2025, katika mafunzo ya uongozi kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa yanayofanyika katika Chuo cha Uongozi mkoani Pwani, Msovela amesema kuwa ushirikiano ni nguzo muhimu katika kufanikisha malengo ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuwaletea wananchi maendeleo ya haraka na yenye tija.
“Ni muhimu tufanye kazi kama timu moja. Miradi ya maendeleo haiwezi kutekelezwa kwa ufanisi ikiwa kila mmoja atafanya kazi kivyake. Ushirikiano, mawasiliano na uwajibikaji ni mambo ya msingi,” amesisitiza Msovela.
Aidha, ameongeza kuwa Makatibu Tawala Wasaidizi wanapaswa kuratibu kwa ufanisi shughuli zote za maendeleo, kufuatilia utekelezaji wake kwa karibu, na kutoa taarifa sahihi kwa wakati ili kusaidia serikali kufanya maamuzi yenye tija.
Msovela amesema viongozi hao ni kiungo muhimu kati ya wananchi na Serikali, hivyo ni lazima wawe karibu na wananchi, kusikiliza changamoto zao na kushirikiana nao katika kuzitafutia suluhisho la kudumu.
Comments
Please sign in to leave a comment.
Matangazo Muhimu
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.
TANGAZO LA KUITWA KAZINI KWA WALIMU WA KUJITOLEA 128 SHULE ZA MSINGI 128 KWA AWAMU YA PILI GPE TSP
ORODHA YA WALIMU WA KUJITOLEA 128 GPE TSP AWAMU YA PILI
ADDITIONAL BEST INDICATORS 2025
BASIC EDUCATION STATISTICS 2025
Generic ESMP for CERC Interventions under DMDP2