
MHE.MCHENGERWA ASHIRIKI KONGAMANO LA UCHUMI LA ARUSHA.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa ni miongoni mwa viongozi waliohudhuria jukwaa la uchumi Arusha linalofanyika katika Ukumbi wa IACC Arusha.
Kongamano hili limejumuisha zaidi ya wadau 1000 kutoka maeneo mbalimbali duniani na kushirikisha mawaziri kadhaa wa sekta za tofauti.
Mwanamajumui wa Afrika Profesa Patrick Lumumba pia amealikwa kuwa miongoni mwa watoa mada.
Jukwaa hilo limeandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Makonda ili kutoa fursa kwa wafanyabiashara wa Mkoa huo kupata ujuzi wa namna ya kutumia fursa za uchumi zilizopo mkoani Arusha.
Comments
Please sign in to leave a comment.
Matangazo Muhimu
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.
TANGAZO LA KUITWA KAZINI KWA WALIMU WA KUJITOLEA 128 SHULE ZA MSINGI 128 KWA AWAMU YA PILI GPE TSP
ORODHA YA WALIMU WA KUJITOLEA 128 GPE TSP AWAMU YA PILI
ADDITIONAL BEST INDICATORS 2025
BASIC EDUCATION STATISTICS 2025
Generic ESMP for CERC Interventions under DMDP2




