
MAHUSIANO MAZURI KATI YA SERIKALI NA TAASISI ZA DINI NI CHACHU KATIKA HUDUMA BORA ZA AFYA.
OR-TAMISEMI
Mkurugenzi wa Idara ya Afya Lishe na Ustawi wa Jamii , Ofisi ya Rais TAMISEMI, Dkt. Rashid Mfaume amesema mahusiano mazuri kati ya Serikali na taasisi za dini yamekuwa chachu katika kufanikisha utoaji wa huduma za afya kwa wananchi.
Dkt. Mfaume ameyasema hayo hivi karibuni mara baada ya kutembelea katika Hospitali ya Cardinal Rugabwa inayomilikiwa na Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam katika ziara yake inayoendelea mkoani huku yenye lengo la kuangalia upatikanaji wa huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii.
“Hapa tunaona mitambo kikubwa ya kutolea huduma za afya, Serikali imeiweka mazingira mazuri ya ushirikiano kati ya Serikali na taasisi za dini zote ikiwa ni pamoja na uwekezaji kwenye Sekta ya afya” amesema Dkt.Mfaume
Aidha, Dkt. Mfaume amezitaka timu za usimamizi wa afya (CHMT) katika Halmashauri kuendelea kufanya kazi kwa ukaribu na taasisi hizo kwa kuwa zinatekeleza majukumu hayo kwa niaba ya Serikali.
Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo Sr.Dkt. Sarah Deogratius amesema ziara ya Mkurugenzi katika Hospitali hiyo imewatia moyo wa kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi.
Comments
Please sign in to leave a comment.
Matangazo Muhimu
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.
TANGAZO LA KUITWA KAZINI WAOMBAJI WA NAFASI YA AJIRA YA MKATABA WA MAAFISA LISHE
CHAGUO LA PILI KIDATO CHA TANO
ORODHA YA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO WALIOPANGWA AWAMU YA PILI MWAKA, 2025
TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI. (ORAL INTERVIEW)
Tangazo la kuitwa kazini ajira za TMCHIP 2025