
LAAC yataka dosari zilizobainishwa na CAG Halmashauri ya Wilaya Kilolo zitatuliwe
Na OR-TAMISEMI, Kilolo
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), imeielekeza Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo kuhakikisha inaziondoa dosari zote zilizobainishwa na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) katika ujenzi wa Shule ya Wasichana ya Lugalo, mkoani Iringa.
Maelekezo hayo yametolewa na Mwenyekiti wa kamati, Halima Mdee baada ya kamati kutembelea na kukagua ujenzi wa shule hiyo.
"Dosari zote zilizobainishwa na CAG katika utekelezaji wa mradi huu zinaondolewa na kuhakikisha miundombinu muhimu inakamilika," amesema Mhe. Mdee.
Kamati pia imeelekeza Afisa Masuuli wa Halmashauri kuandaa taarifa yenye maelezo ya kina na mchanganuo wa matumizi ya fedha zote za mradi huo na kuiwasilisha kwa CAG kwa ajili ya uhakiki.
Aidha, kamati imeitaka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kufanya tathmini ya kina na kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa mradi huo, huku ikichukua hatua za haraka iwapo kutabainika ukiukwaji wa sheria na taratibu.
Comments
Please sign in to leave a comment.
Matangazo Muhimu
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.
TANGAZO LA KUITWA KAZINI KWA WALIMU WA KUJITOLEA 128 SHULE ZA MSINGI 128 KWA AWAMU YA PILI GPE TSP
ORODHA YA WALIMU WA KUJITOLEA 128 GPE TSP AWAMU YA PILI
ADDITIONAL BEST INDICATORS 2025
BASIC EDUCATION STATISTICS 2025
Generic ESMP for CERC Interventions under DMDP2