
Laac yaagiza ujenzi wa hospitali ya mji ifakara ukamilike
Na OR-TAMISEMI, Ifakara
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), imeielekeza Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara kuhakikisha ujenzi wa hospitali ya mji huo unakamilika kwa wakati ili wananchi wapate huduma bora za afya.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Halima Mdee, ametoa maelekezo hayo baada ya kutembelea na kukagua miradi miwili ya maendeleo ambayo ni ujenzi wa jengo la utawala na ujenzi wa hospitali ya Mji wa Ifakara.
"Afisa Masuuli aondoe dosari zote zilizobainishwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ili mradi huu ukamilike na kutoa huduma kamili kwa wananchi. Aidha, taarifa ya kila robo mwaka ya maendeleo ya ujenzi huu iwasilishwe kwa CAG kwa ajili ya uhakiki," amesisitiza Mhe. Mdee.
Pia, amemtaka Afisa Masuuli kuhakikisha kuwa zaidi ya Sh. milioni 133, ambazo zilichukuliwa kutoka kwenye fedha zilizotolewa na Serikali Kuu kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo, zinarudishwa ili kuendeleza mradi huo.
Vilevile, Mhe. Mdee ameelekeza kuwa utekelezaji wa miradi katika halmashauri hiyo uzingatie sheria, kanuni, na miongozo inayotolewa na Ofisi ya Rais – TAMISEMI.
Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Atupele Mwambene, amesema kuwa ofisi yake imepokea maelekezo hayo na itahakikisha yanatekelezwa kikamilifu kwa usimamizi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara.
Comments
Please sign in to leave a comment.
Matangazo Muhimu
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.
TANGAZO LA KUITWA KAZINI KWA WALIMU WA KUJITOLEA 128 SHULE ZA MSINGI 128 KWA AWAMU YA PILI GPE TSP
ORODHA YA WALIMU WA KUJITOLEA 128 GPE TSP AWAMU YA PILI
ADDITIONAL BEST INDICATORS 2025
BASIC EDUCATION STATISTICS 2025
Generic ESMP for CERC Interventions under DMDP2




