
Katimba: Serikali imeendelea kuchukua hatua kupunguza uhaba wa walimu
Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Zainab Katimba, amesema serikali inaendelea kuchukua hatua za kukabiliana na upungufu wa walimu kwa kuajiri kila mwaka kulingana na upatikanaji wa fedha, huku kwa sasa ikiwa katika majaribio ya matumizi ya teknolojia ya madarasa janja.
Mhe. Katimba ameyasema hayo leo, Februari 22, 2025, alipokuwa akizungumza na Maofisa Elimu Kata waliokuwa wakipatiwa mafunzo ya matumizi ya Madarasa Janja katika Taasisi ya Elimu Kibaha, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kutembelea taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Rais – TAMISEMI.
Amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuajiri walimu kila mwaka kwa kutoa vibali vya ajira, huku ikiimarisha utaratibu wa kuwatumia walimu wa kujitolea.
"Watanzania wamehamasika kupeleka watoto shule, na udahili wa wanafunzi umeongezeka maradufu, hali iliyosababisha upungufu wa walimu. Hivyo, serikali, pamoja na kuajiri, imebuni teknolojia ya kutumia madarasa janja, na kwa sasa ipo katika hatua za majaribio," amesema.
Pia, Mhe. Katimba amebainisha kuwa pamoja na jitihada hizo, serikali inaendelea kupandisha madaraja ya walimu kama sehemu ya motisha ya kiutendaji.
Comments
Please sign in to leave a comment.
Matangazo Muhimu
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.
TANGAZO LA KUITWA KAZINI KWA WALIMU WA KUJITOLEA 128 SHULE ZA MSINGI 128 KWA AWAMU YA PILI GPE TSP
ORODHA YA WALIMU WA KUJITOLEA 128 GPE TSP AWAMU YA PILI
ADDITIONAL BEST INDICATORS 2025
BASIC EDUCATION STATISTICS 2025
Generic ESMP for CERC Interventions under DMDP2