
Katimba atembelea banda la TAMISEMI kwenye Kongamano la Kimataifa na Maonesho ya Elimu Mtandao Jijini Dar es Salaam
Naibu Waziri anayeshughuhulikia Elimu Ofisi ya Rais - TAMISEMI Mhe.Zainab Katimba atembelea banda la TAMISEMI kwenye Kongamano la Kimataifa na Maonesho ya Elimu Mtandao Jijini Dar es Salaam.
Mheshimiwa Zainab Katimba ametembelea banda la maonesho la Ofisi ya Rais -TAMISEMI kwenye Kongamano la 18 la kimataifa na Maonesho ya Elimu Mtandao, Mafunzo na Maendeleo ya Kukuza Ujuzi yanayoendelea katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam kuanzia leo Mei 7 hadi 9, 2025.
Mheshimiwa Katimba amejionea jinsi Mfumo wa Taarifa za Shule (SIS) unavyofanya kazi kwa kukusanya taarifa za shule za kila siku kupitia moduli mbalimbali zilizounganishwa na Mfumo huo.
Pia amepata maelezo ya namna ya darasa janja (smart class) linavyofanya kazi za kufundisha na kutoa mafunzo kama sehemu ya Elimu Mtandandao (eLearning).
Maonesho na Kongamano hilo la Elimu Mtandao yanajulikana kama “eLearnging Africa’ yanafanyika kwa mara ya pili Tanzania na mara ya kwanza yalifanyika mwaka 2007, yameandaliwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ikiwahusisha wadau mbalimbali kutoka Wizara, Taasisi, Mashirika ya Kimataifa na Wadau wengine na Kauli Mbiu yake ni “Kufikiri Upya Elimu na Maendeleo ya Rasilimali Watu kwa ustawi wa Baadae wa Afrika”
Comments
Please sign in to leave a comment.
TANGAZO LA KUITWA KAZINI KWA WALIMU WA KUJITOLEA 128 SHULE ZA MSINGI 128 KWA AWAMU YA PILI GPE TSP
ORODHA YA WALIMU WA KUJITOLEA 128 GPE TSP AWAMU YA PILI
ADDITIONAL BEST INDICATORS 2025
BASIC EDUCATION STATISTICS 2025
Generic ESMP for CERC Interventions under DMDP2