
DC CHAMWINO AHIMIZA ELIMU YA MFUMO WA TAUSI KWA WANANCHI.
Na Angela Msimbira – OR-TAMISEMI
Mkuu wa Wilaya ya Chamwino, Bi. Janet Mayanja, ametoa wito kwa Ofisi ya Rais – TAMISEMI kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi ya Mfumo wa Tausi ili kuongeza uelewa, kuimarisha uwajibikaji na kukuza ushirikiano kati ya Serikali na wananchi.
Akizungumza mara baada ya kutembelea banda la Ofisi ya Rais – TAMISEMI katika Maonesho ya Kilimo ya Nanenane yanayofanyika katika viwanja vya Nzuguni, Mkoani Dodoma, Bi. Janet amesema bado kuna uelewa mdogo miongoni mwa wananchi kuhusu mfumo huo mpya wa kidijitali.
“Ni muhimu wananchi wakaelewa dhima ya mfumo huu na namna unavyoweza kuwawezesha kupata huduma kwa haraka, uwazi na kwa ufanisi mkubwa zaidi,” amesisitiza Bi. Janet.
Ameongeza kuwa elimu endelevu kwa umma ni muhimu ili kuhakikisha mfumo wa Tausi unatekelezwa kikamilifu na kwa mafanikio, hasa katika ngazi ya Serikali za Mitaa.
Mfumo wa Tausi ni jukwaa la kidijitali linalolenga kuboresha uratibu wa taarifa, utoaji wa huduma na kuongeza uwajibikaji katika utendaji kazi wa Serikali za Mitaa kwa kutumia teknolojia ya kisasa.
Comments
Please sign in to leave a comment.
Matangazo Muhimu
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.
TANGAZO LA KUITWA KAZINI KWA WALIMU WA KUJITOLEA 128 SHULE ZA MSINGI 128 KWA AWAMU YA PILI GPE TSP
ORODHA YA WALIMU WA KUJITOLEA 128 GPE TSP AWAMU YA PILI
ADDITIONAL BEST INDICATORS 2025
BASIC EDUCATION STATISTICS 2025
Generic ESMP for CERC Interventions under DMDP2




